Flatnews

HABARI/PICHA:- MOTO WATEKETEZA SOKO URAMBO MKOANI TABORA


aloyson.com 
Moto uliowaka zaidi ya masaa 9 umeteketeza meza zaidi ya 250 na maduka zaidi ya 330 ya wafanyabiashana, huku wananchi wakihangaika kuuzima kwa kutumia mchanga, katika soko kuu la mji mdogo wa Urambo mkoni Tabora usiki wa kuamkia leo, katika kile, kilichohisiwa kuwa, unaweza kuwa umesababishwa na mamarishe ndani ya soko.

Wakiongea kwa masikitiko baadhi ya wafanyabiashara walioathiriwa na moto huo, katika soko hilo wameiomba serikali kujitahidi kuwatenda akinamamarishe na mafundi wa kushona nguo kuwaondoa katikati ya maduna na meza kwani inawezekana kuwa, waliacha moto ukiwaka, na kusababisha hasara ya mamiliono ambayo haikupatikana mara moja.
 aloyson.com

Aidha akizungumzia changamoto iliyowakumba wananchi wa kata hiyo kutokana na hasara ya mamilioni, waliyoipata, diwani wa kata hiyo ya urambo mjini Bw. Amatus Liumba ameliomba wananchi kujenga tabia ya uaminifu kwani katika kuokoa mali nyingi zilihamia katika njia za panya na kutoweka. 
Juhudi za kumpata afisa biashara wa wilaya Bw. Hatibu Abdulahamani ili kujua kiasi hasara walioipa wafanya bishara hao zinaendelea kutokana na tathimini zinazoendelea kufanyika.

Post a Comment

emo-but-icon

item