MTOTO ALIYEZAMIA KWEYE NDEGE, ATOWEKA TENA NYUMBANI! SOMA ZAIDI HAPA!
https://samchardtz.blogspot.com/2014/09/mtoto-aliyezamia-kweye-ndege-atoweka.html
Mtoto Happiness Rioba(10) aliyedaiwa kuzamia kwenye ndege kutoka Dar es Salaam kwenda Zanzibar bila kugundulika, ametoweka tena nyumbani kwao baada ya kukutanishwa na mama yake mzazi Sara Zefhania.
Happiness
ambaye ni mkazi wa eneo la Mkokozi, Wilaya ya Mkuranga mkoani Pwani
inadaiwa ametoweka katika mazingira ya kutatanisha.
Akizungumza na Mwananchi jana, Sara alisema mwanawe alitoweka jana saa sita mchana na kutokomea kusikojulikana.
Alisema asubuhi mtoto wake aliamka salama bila tatizo lolote na muda wote walikuwa
pamoja kwa kuwa alikuwa na wageni kutoka kituo cha televisheni cha ITV,
waliomuahadi kumtembelea nyumbani kwa lengo la kumuona Happiness.
“Aliamka vizuri tu na muda wote alikuwapo nyumbani, lakini ilipofika saa sita mchana, nilipigiwa simu na waandishi wa habari wa ITV kuwa nikawachukue katika kituo cha daladala... kabla sijaondoka nilimwambia mwanangu nakwenda kupokea wageni, lakini niporejea nyumbani na wageni hatukumkuta,”
alisema Sara.
Alisema baada ya kumkosa alianza kumtafuta akishirikiana na waandishi hao pamoja na majirani,
lakini hawakufanikiwa kumpata ndipo alipotoa taarifa kwa mjumbe wa
Serikali za Mitaa na kuwataarifu ndugu, jamaa na marafiki.
Aidha, aliongeza
mwanawe alipokuwa Zanzibar alifanya mambo ya ajabu likiwamo kuongea na
paka, kula chakula kwa kutumia mkono wa kushoto, kutokuongea na watu
pamoja na kutoweka katika mazingira ya kutatanisha.
