Mapigano makali yaanza tena Sudan Kusini
https://samchardtz.blogspot.com/2014/05/mapigano-makali-yaanza-tena-sudan-kusini.html
Mapigano makali yamekuwa
yakiendelea katika mji wa Bentiu nchini Sudan Kusini ambapo vikosi vya
serikali vinajaribu kuurejesha mji huo uliotekwa na waasi.
Mwandishi wa Habari wa BBC aliyeandamana na
kikosi cha Umoja wa Mataifa nje ya mji huo anasema amesikia milio ya
bunduki na silaha nzito nzito ambapo pia ameona kikosi cha majeshi ya
serikali kikijipanga.Kwa upande serikali nchini Sudan kusini inasema majeshi yake yameudhibiti mji wa huo na ngome ya waasi ya Nasir.
Baadhi ya wakimbizi wa Sudan Kusini waliokimbia makazi yao hivi karibuni kutokana na vita
Shambulio hilo linajiri siku mbili baada ya rais Salva Kiir kumwambia Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani John Kerry, kwamba yupo tayari kufanya mazungumzo ya amani ya moja kwa moja na kiongozi wa waasi, Riek Machar.