Flatnews

CHAGUO LA GK : 'NOT FORGOTTEN' YA WATOTO CHILDREN CHOIR UGANDA

Nikiwa na Watoto Children Choir no 58 mwaka jana Big Church Day Out (BCDO) Uingereza.


Nikiwa na Watoto Children Choir no 58 mwaka jana Big Church Day Out (BCDO) Uingereza.
Chaguo la GK Jumapili ya leo zinakwenda kwa kwaya ya Watoto Children Choir kutoka nchini Uganda, ambao ni maarufu duniani kwakazi yao njema ya kumtukuza Mungu. Mpaka sasa ni zaidi ya kwaya 60 zimekuwepo toka kundi la kwanza lililoanza mwaka 1994 mpaka hii leo, ambapo kwa mwaka makundi ya kwaya hugawanywa kufanya ziara za kihuduma katika mabara mbalimbali, awali hutangulia kwa kufanya matamasha kanisani kwao Uganda kuonyesha kile walichojifunza mda wote kabla ya kuanza ziara hizo.

Kwaya hii ya watoto ambao wengi wao walitelekezwa na wazazi wao, wengine wakiwa yatima kutokana na vita kaskazini mwa Uganda huku wengine wakiachwa yatima kutokana na wazazi wao kufariki kwa gonjwa la ukimwi, wamekuwa wakilelewa chini ya kanisa la Watoto ambalo ibada zao huendeshwa kwa namna ya kanisa la Hillsong.

Kutoka katika kwaya hii tumekuchagulia wimbo maarufu kutoka kwao uitwao 'Not Forgotten'. Natumai utakuwa na jumapili njema kwamba licha ya yote unayopitia, kukosa wazazi, marafiki, furaha, amani lakini bado Mungu wa mbinguni hajakusahau, maana alikukomboa na anakujua kwa jina lako. Furahi sasa

Post a Comment

emo-but-icon

item