Ziara hiyo ya Cameron ilikuwa ya mwisho kabla timu hiyo haijachuana Peru na kuondoka kwelekea kwenye kipute hicho kitakachoanza tarehe 12 mwezi ujao huko Brazil.

Cameron aitembelea timu ya Kombe la dunia
Mkufunzi Hodgson amedhibitisha kwamba kikosi chake hakina matatizo ya majeraha ingawa Shaw anaugua.
Beki huyo mwenye umri wa miaka 18 aliichezea Uingereza mechi yake ya kwanza katika mchuano wa kirafiki dhidi ya Denmark mnamo mwezi Machi na kutajwa miongoni mwa wachezaji 23 watakaoshiriki kombe la dunia.
Tangu alipoanza kushiriki mechi za kimataifa, Shaw anadaiwa kuvutia vilabu kadhaa Uingereza, huku Manchester United ikidaiwa kutoa fedha za kutaka kumsajili.