BREAKING NEWS: MCHUNGAJI WA UFUFUO NA UZIMA ALISHWA SUMU
Mchungaji Omari katika mojawapo ya mafundisho Ufufuo na Uzima, Kawe jijini Dar es Salaam. Wimbi la mashambulizi kwa viongozi mba...
https://samchardtz.blogspot.com/2014/04/breaking-news-mchungaji-wa-ufufuo-na.html
| Mchungaji Omari katika mojawapo ya mafundisho Ufufuo na Uzima, Kawe jijini Dar es Salaam. |
Wimbi la mashambulizi kwa viongozi mbalimbali na makanisa nchini
yakiendelea kusikika kama ya kawaida masikioni mwa wananchi, taarifa
ambazo zimefikia Gospel Kitaa ni kwamba Mchungaji Omary Juma almaarufu
kwa jina la Sheikh Omary Juma, amelazwa kwenye hospitali ya Aga Khan ya
jijini Dar es Salaam baada ya kulishwa sumu.
Kwa mujibu wa taarifa zilizotolewa kwa ufupi kwenye kundi la wanaufufuo na uzima
kwenye ukurasa wa kijamii wa facebook, imeelezwa kuwa mchungaji huyo
amelishwa yuko hospitalini kwa ajili ya uchunguzi na matibabu zaidi,
ambapo pia haijafahamika kwa hivi sasa mchungaji huyo wa kanisa la
Ufufuo na Uzima ambaye pia hivi karibuni alikuwep kwenye ibada ya
ubatizo ya kanisa hio jijini Arusha anaendeleaje.