Flatnews

Obama, Kenyatta kuwajadili Al shabaab

Rais wa Marekani Barack Obama akiwa na bibi yake Mama Sarah Obama kushoto na dada yake Auma Obama katika chakula cha jioni na wanandug...


Rais wa Marekani Barack Obama  akiwa na bibi yake  Mama Sarah Obama kushoto na dada yake  Auma Obama katika chakula cha jioni na wanandugu wa familia ya Obama nchini Kenya
Rais wa Marekani Barack Obama akiwa na bibi yake Mama Sarah Obama kushoto na dada yake Auma Obama katika chakula cha jioni na wanandugu wa familia ya Obama nchini Kenya.



Rais wa Marekani Barack Obama aliyewasili nchini Kenya anatarajia kukutana na Rais Uhuru Kenyatta  kwa mazungumzo ambapo wataangazia usalama wa kanda hiyo na tisho kutoka kwa kundi la kigaidi la Al shabaab.
Miongoni mwa mambo mengine atakayoa angazia ni kuhutubia kongamano la wajasiriamali pamoja na masuala ya ufisadi ulioitikisa nchi hiyo na kupelekea vigogo kadhaa kusimamishwa kazi.
Rais Obama baadaye atatembelea eneo kulikotokea shambulizi la kigaidi katika uliokuwa ubalozi wa marekani mjini Nairobi na pia kukutana na rais wa kenya uhuru.
Nchi  ya  Marekani imekuwa ikiisadia kenya katika vita dhidi ya ugaidi na imewaua vongozi kadha wa kundi la al shabaab kwenye mashambulizi ya ndege zisizokuwa na rubani.

Related

NEWS 3951822914394118750

Post a Comment

emo-but-icon

item