Flatnews

Man Utd Kupanda Hadi Nafasi Ya Tatu



Man Utd Kupanda Hadi Nafasi Ya Tatu 
Ligi kuu ya soka nchini Uingereza itaendelea tena hii leo kwa mchezo mmoja ambapo mabingwa wa kihistoria kwenye ligi hiyo Man Utd watakuwa ugenini huko The Hawthorns wakipepetana na West Bromwich Albion.
Man Utd wataingia uwanjani hii leo huku wakijiamini kutokana na mambo kuwaendelea vyema katika mchezo wao uliopita ambapo waliibanjua Everton mabao mawili kwa moja katika uwanja wao wa nyumbani wa Old Trafford.
Kwa upande wa West Bromwich Albion wao watakuwa wakikumbukia kisago cha mabao mawili kwa moja walichokipokea kutoka kwa majogoo wa jiji Liverpool, hivyo hawatokuwa tayari kuangusha point nyingine tatu kwa mara ya pili mfululizo.
Endapo Man Utd watafanikisha suala la ushindi hii leo watachupa hadi kwenye nafasi ya tatu katika msimamo wa ligi kuu ya soka nchini Uingereza.

Post a Comment

emo-but-icon

item