Mazoezi Yanga sasa ni kimya kimya!
http://samchardtz.blogspot.com/2014/08/mazoezi-yanga-sasa-ni-kimya-kimya.html
Kocha Mkuu wa Yanga, Marcio Maximo
By LASTECK ALFRED
(email the author)
- Kocha Mkuu wa Yanga, Marcio Maximo amesema kuwa waandishi na watu wengine wachache wataruhusiwa kuangalia kidogo na kuzungumza naye siku ya Ijumaa tu. Bosi huyo amesisitiza kuwa anafanya hivyo ili kuficha siri zake na watu wasione mbinu zake kwani mambo yanavuja sana na hata wapinzani wao wanawasoma sana kiufundi.
YANGA itakwenda Zanzibar keshokutwa Jumatatu
kuweka kambi ya siku 10, lakini ikirejea Dar es Salaam kila kitu
mazoezini kitakuwa siri na hakuna yeyote atakayeruhusiwa kushuhudia kama
si mchezaji. Itakuwa hivyo hata kwa viongozi.
Kocha Mkuu wa Yanga, Marcio Maximo amesema kuwa
waandishi na watu wengine wachache wataruhusiwa kuangalia kidogo na
kuzungumza naye siku ya Ijumaa tu. Bosi huyo amesisitiza kuwa anafanya
hivyo ili kuficha siri zake na watu wasione mbinu zake kwani mambo
yanavuja sana na hata wapinzani wao wanawasoma sana kiufundi.
Kambi hiyo ya visiwani Pemba ni sehemu tu ya maandalizi ya Ligi Kuu Bara na mechi ya Ngao ya Hisani dhidi ya Azam FC.
“Ninapenda kuwaomba radhi waandishi wa habari
pamoja na wapenzi wa Yanga ambao wamekuwa wakifuatilia mazoezi kila mara
kwa kuwa hawataweza kuona kinachoendelea mazoezini kwa takribani wiki
tatu tukitoka Pemba,” alisema.
“Kuna vitu ni siri na kuna mbinu na mafunzo
maalumu ambayo nitawapa wachezaji wangu ambavyo havitakiwi kuonekana na
mtu yeyote nje ya kikosi.
“Lengo langu ni kuwa na timu pamoja kwa karibu na
kuwapa ujuzi wa ziada ambao utakuwa na manufaa kwa timu na itakuwa siri
ya mafanikio yetu.”
Mara kadhaa makocha mbalimbali wamekuwa
wakitiririka kuangalia mazoezi anayotoa Maximo kwa wachezaji wake kwenye
Uwanja wa Shule ya Sekondari wa Loyola jijini Dar es Salaam baadhi ya
makocha kama Mbwana Makatta, Shija Renatus waliwahi kuhudhuria na kuona
mbinu hizo.
Maximo alisema: “Nahitaji usiri ili vitu ambavyo
nitafundisha viwe na manufaa. Nataka kufanya kama Ufaransa na Ujerumani
wakati wa Kombe la Dunia, hawa walikuwa hawaonyeshi mbinu zao, nikienda
na mfumo huo ndiyo nitaweza kufika mbali, Brazil ilikwama kwa sababu ya
kuonesha mbinu mbalimbali ambazo baadaye wapinzani wao walizisoma.”
Yanga imepanga kucheza mechi mbili za kirafiki
wakati itakapokuwa Pemba ili kuanza kuwapa wachezaji wake uzoefu wa
mechi za ushindani na pia kumsaidia Maximo kupata kikosi cha kwanza.
Maximo aliongeza: “Jaja anajitahidi siku hadi
siku, nina furaha kuwa mambo yanaenda vizuri. Tatizo kubwa ni kuwa yeye
na Coutinho (Andrey) walikuja Tanzania wakiwa hawapo kwenye viwango vyao
baada ya kuwa nje ya uwanja kwa ajili ya mapumziko kwani ligi ya Brazil
ilikuwa imekwisha.”
Awapa mbinu mastraika
Maximo anaonekana kuamini kombinesheni ya mastaika
Jerry Tegete na Jaja na kwa hilo amewapa mbinu za jinsi ya
kuwachanganya mabeki wa timu pinzani.