Urasimu bandarini Mombasa kushughulikiwa
http://samchardtz.blogspot.com/2014/06/urasimu-bandarini-mombasa-kushughulikiwa.html
Mashirika 25 yanayohudumu kazi katika Bandari ya Mombasa leo yanatia saini mkataba wa ushirikiano unaolenga kupunguza hasara ya mabilioni ya dola itokanayo na urasimu katika Bandari hiyo.
Kumekuwa na utaratibu mrefu wa kusafirisha na kupokea bidhaa kutoka bandari ya Mombasa inayotegemewa na nchi za Afrika Mashariki na kati, hususan kwa shehena za mizigo kutoka mataifa ya ng'ambo.
Mkataba huo unaazimia kupunguza siku za ukaguzi wa shehena zinzoingia na kutoka kwenye bandarini hiyo, na kupunguza malalamiko ya wafanyabiashara wanaoagiza bidhaa kupitia bandari ya Mombasa.
CHANZO NI BBC SWAHILI
