Flatnews

Uhispania yaaga Brazil2014

Uhispania iliilaza Australia 3-0


Uhispania iliilaza Australia 3-0

Mabingwa watetezi wa kombe la dunia Uhispania waliepuka fedheha ya kukamilisha mechi za makundi za mchuano wa Brazil 2014 katika nafasi ya mwisho kwa kuilaza Australia mjini Curitibia.
Mabao ya Uhispania yalifungwa na David Villa, Fernando Torres na Juan Mata.
Villa alifunga bao la kwanza kutoka na pasi yake Juanfran, kabla ya mshambulizi wa Chelsea Torres kufunga la pili.
Mata alifunga la tatu kutoka kwenye pasi ya mchezaji aliyekuwa wa ziada Cesc Fabregas.
Vijana wa Vicente del Bosque sasa wamemaliza katika nafasi ya tatu wakiwa na alama tatu baada ya kushindwa mara mbili na kushinda mechi moja.
Haya ndiyo matokeo yao mabay zaidi tangu mwaka wa 1991.

Post a Comment

emo-but-icon

item