KWELI NDOA NI TAMU, AUNT LULU ALILIA BWANA
MKALI wa sinema za Kibongo, Lulu Semagongo ‘Aunt Lulu’ amefunguka kuwa anasikitika kukosa bwana aliyeahidiwa na marehemu Amina Ngaluma. ...
http://samchardtz.blogspot.com/2014/06/kweli-ndoa-ni-tamu-aunt-lulu-alilia.html
MKALI wa sinema za Kibongo, Lulu Semagongo ‘Aunt Lulu’ amefunguka kuwa anasikitika kukosa bwana aliyeahidiwa na marehemu Amina Ngaluma.
Akizungumza
na paparazi wetu, Aunt Lulu alisema kabla marehemu Amina hajapatwa na
mauti nchini Thailand, alimuahidi kumtafutia bwana nchini humo lakini
mauti yalimkuta kabla hajamtimizia ahadi hiyo.
“We
acha tu, aliniahidi kunitafutia mume baada ya kugundua nasumbuliwa na
wanaume kila wakati lakini ndiyo hivyo tena Mungu akamchukua kabla
hajanitimizia ahadi,” alisema Aunt Lulu.
Amina alifariki mwezi uliopita nchini humo ambapo chanzo cha kifo chake kikielezwa kuwa ni uvimbe kwenye kichwa.
Amina alifariki mwezi uliopita nchini humo ambapo chanzo cha kifo chake kikielezwa kuwa ni uvimbe kwenye kichwa.