SIMULIZI YA RECHO INAUMA
HUKU makovu ya machungu ya kifo cha msanii wa filamu za Kibongo, Rachel (Sheila) Leo Haule ‘Recho’ yakiwa bado hayajakauka, Risasi si l...
http://samchardtz.blogspot.com/2014/05/simulizi-ya-recho-inauma.html
HUKU makovu
ya machungu ya kifo cha msanii wa filamu za Kibongo, Rachel (Sheila)
Leo Haule ‘Recho’ yakiwa bado hayajakauka, Risasi si linakupa simulizi
yenye maumivu kuhusu marehemu huyo.
Recho
alifariki dunia Mei 27, mwaka huu katika Hospitali ya Taifa Muhimbili
alipokuwa amelazwa kwenye chumba cha wagonjwa wanaohitaji uangalizi
maalum ‘ICU’ baada ya kujifungua na mtoto kufariki dunia muda mfupi
baadaye.
Staa huyo alijifungua kwa upasuaji mtoto wa kiume, lakini kwa bahati mbaya tatizo la presha ya kushuka na sukari lilimpata na hivyo kuanza kupatiwa huduma ya haraka kabla ya mauti kumkuta.
Recho alijifungua katika Hospitali ya Rufaa ya Jeshi Lugalo, Jumapili Mei 25, mwaka huu na hali ilipobadilika alikimbizwa Muhimbili, kabla ya mauti kumfika.
Staa huyo alijifungua kwa upasuaji mtoto wa kiume, lakini kwa bahati mbaya tatizo la presha ya kushuka na sukari lilimpata na hivyo kuanza kupatiwa huduma ya haraka kabla ya mauti kumkuta.
Recho alijifungua katika Hospitali ya Rufaa ya Jeshi Lugalo, Jumapili Mei 25, mwaka huu na hali ilipobadilika alikimbizwa Muhimbili, kabla ya mauti kumfika.
SIMULIZI YENYEWE
Mchumba anayeonekana ni mume wa marehemu Recho, George Saguda ambaye uhusiano wao ni wa miaka takribani mitano sasa, alisimulia mazito kuhusu uhusiano wake na marehemu huyo.
“Nina machungu sana moyoni.
Naumia kumpoteza mke wangu na mwanangu. Walikuwa muhimu sana kwangu. Ndoto zote zimezimika. Ulikuwa mwanzo mzuri wa maisha yetu tuliyokuwa tumeyapanga,” alisema Saguda.
Akaongeza:
“Sikuwa na hili wala lile. Taarifa za kifo cha Recho bado kama ndoto, ningefurahi kama ingekuwa hivyo. Tulipanga mengi na Recho, sikujua kama mwisho wake ulikuwa umefika.”
“Tulijiandaa vizuri sana kumpokea mtoto wetu. Siku chache kabla ya kusikia uchungu, tulikwenda madukani kumfanyia mtoto shopping. Tulitumia zaidi ya shilingi laki nane (800,000).
“Tulimchagulia nguo nzuri na vitu vingine muhimu kwa ajili yake, kumbe Mungu alikuwa ameshapanga yake (analia).”
SIMANZI TUPU
“Tulimfikisha Recho salama Hospitali ya Lugalo, akajifungua vizuri mtoto wa kiume. Nakumbuka ilikuwa Jumapili usiku. Lakini kutokana na hali ya mtoto ilivyokuwa, hakupewa. Aliwekwa chini ya uangalizi wa manesi.
“Mke wangu hakuwa na hali mbaya ya kutisha, niliondoka hospitalini na tukawa tunatumiana meseji ule usiku. Ni picha ambayo inagoma kufutika kichwani mwangu.”
“Kuna meseji alinitumia, akasema: Mume wangu nimekuzalia kidume, naona sasa utakuwa umepata mtu wa kwenda naye uwanjani kushangilia mpira, siku Yanga ikicheza.
“Meseji hiyo inaniumiza sana. Nashindwa kuamini kilichoendelea, moyo wangu una majonzi sana. Ni ngumu kukubali kifo kilichotokea usiku wa Jumatatu wakati Jumapili tu nilikuwa nachati naye. Sijielewielewi kwa kweli.”
WASIWASI
Anasema usiku wa Jumapili akiwa wodini, alimwangalia Recho na kuona namna hali yake ilivyobadilika, akamwambia: “Mke wangu naona kama hali yako siyo nzuri, umechoka sana lakini jikaze, utapata nafuu tu.”
MIPANGO YA MAISHA
Akizidi kumzungumzia marehemu, Saguda alisema Recho alikuwa mwanamke sahihi katika maisha yake kwani walipanga mengi na walianza kutekeleza kwa msaada mkubwa wa mawazo yake.
“Alikuwa mwanamke mwenye akili sana. Recho si mfujaji wa fedha. Unaweza kuacha shilingi milioni kumi (10,000,000) ndani asipate tamaa ya kuziingiza kwenye matumizi ambayo hayakuwa kwenye mipango.
Tulikuwa tupo kwenye mipango ya kuanza kurekodi filamu nyingine.
“Alikuwa mwanamke anayeangalia maendeleo zaidi, hakupenda sana starehe. Kuna wakati nilimwambia sasa tununue gari, akasema hapana, tujijenge kwanza ndipo tununue gari, tena yeye akasema inafaa tununue Noah (Toyota) ili litusaidie pia location (shughuli za kurekodi).